Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, October 30, 2013

WAFANYAKAZI WA KIWANDA CHA KONYAGI (TDL) WALIOKWENDA KUONA MECHI YA BARCELONA NA REAL MADRID,HISPANIA WAREJEA WAKIWA NA BASHASHA TELE


Mfanyakazi wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), Khadija Madawili ambaye alikuwa kiongozi wa msafara wa wafanyakazi wa TDL waliokwenda kushuhudia pambano la Ligi ya La Liga ya Hispania kati ya Barcelona na Rael Madrid, akirejea jana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam. Wafanyakazi watano wa TDL, waliteuliwa baada ya kampuni hiyo kushinda  Tuzo ya SABMILLER AFRICA MB COMPLEMENTARY BEVERAGE CATEGORY AWARD FOR F 13)
 Joseph Chibehe (kushoto) akilakiwa na mkewe baada ya kuwasili
                                             Chibehe akiwa na furaha baada ya kulakiwa na mkewe
 Bavon Ndumbati (kushoto), akilakiwa na ndugu yake. Katikati ni Michael Mrema
                                                              Bavon akiwa na furaha
                                                                 Mwesiga Mchuruza.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Konyagi ya Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa (katikati), akiwa na mabosi wa kampuni mama ya SABMILLER AFRICA.wakiwa wameshikilia tuzo hiyo ya  MB COMPLEMENTARY BEVERAGE CATEGORY AWARD FOR (F 13).

KAMPUNI ya Tanzania Distilleries Ltd, (KONYAGI) ambayo ni miongoni mwa kampuni tanzu za Kampuni ya Sabmiller South Africa, imeshinda tuzo ya utendaji bora wa bidhaa (SABMILLER AFRICA MB COMPLEMENTARY BEVERAGE CATEGORY AWARD FOR F 13). Sabmiller inamiliki zaidi ya viwanda 60 vya bia na vinywaji vingine duniani.

Baada ya ushindi huo, Mkurugenzi Mkuu wa TDL, Mgwassa ambaye alipambana mpaka kupata ushindi huo, aliamua kuwazawadia baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo, kwenda Hispania kushuhudia pambano la timu kubwa za Barcelona na Real Madrid lililofanyika mwishoni mwa wiki.

Wafanyakazi waliokwenda Hispania  na kurejea jana usiku kwa ndege ya Afrika Kusini ni; Joseph Chibehe, Khadija Madawili, Bavon Ndumbati, Michael Mrema na Mwesiga Mchuruza.

Wafanyakazi hao, walipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, walionekana kuwa na bashaha na kupokelewa na ndugu zao pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzao.

Akizungumza kwa niaba ya wenzie,Michael Mrema wa Kanda ya Kaskazini, alisema kuwa wanashukuru uongozi kuwapa zawadi hiyo, ambayo imewafanya kuwa na morari mpya wa kazi.

Pia anaseama walifurahi sana kushuhudia mechi hiyo kubwa ya timu za Barcelona na Real Madrid ambapo timu ya Barcelona waliyokuwa wanaishabikia kushinda mabao 2-1.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...