Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, January 31, 2011

CHANETA NA CHANEZA ZAKUTANA NA BMZ PAMOJA NA BMT

Mwenyekiti wa CHANETA ANNA BAYA wa kwanza kushoto akifuatiwa na makamu mwenyekiti SHY ROSE BHANJI pamoja na Katibu msaidizi ROSE MKISI.

Vyama vya netiboli TANZANIA BARA na VISIWANI vimekutanishwa na mabaraza ya michezo BARA na VISIWANI ili kumalizi migogoro katika vyama hivyo ambavyo vimekuwa katika mgogoro kwa muda mrefu.

Mkutano huo umewakutanisha wajumbe kutoka CHANEZA na CHANETA chini ya BMZ na BMT ambapo mwenyekiti wa baraza la michezo nchini IDD KIPINGU amesema sheria kali itachukuliwa iwapo vyama hivyo havitamaliza migogoro

Kutokana na migogoro katika vyama hivyo wanashindwa kushirikiana katika kuandaa timu ya TAIFA ya netiboli pindi inapohitajika kushiriki katika mashindano mbalimbali.

Mshindano ya ligi ya muungano yameshindwa kufanyika kutokana na migogoro ambayo inaendelea katika vyama hivyo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...