Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, January 31, 2011

KAMPUNI YA TRUCKS YAKABIZI MALORI YA TAKA MANISPAA YA ILALA

Mkurugenzi wa Kampuni ya G.F Trucks & Equipment Ltd, Imran Karmal (kushoto) akimkabidhi mfano wa funguo, Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Slaa, wakati wa hafla fupi ya kukabidhi malori sita ya kuzolea taka kila moja likiwa na thamani ya Sh. Milioni 115 kwa Manispaa hiyo, wakati wa hafla hiyo iliyofanyika kwenye ofisi za kampuni hiyo Barabara ya Nyerere Dar es Salaam leo mchana. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni hiyo, Mehboob Karmal. Wapili (kushoto) ni Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Jamii na Uchumi, Angela Malembeka.
Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya G.F Trucks & Equipment Ltd, Mehboob Karmal (kulia) akimuonyesha Meya wa Manispaa ya Ilala, Jrry Slaa, Malori manne kati ya sita, yaliyotolewa na kampuni hiyo kwa Manispaa ya Ilala kwa ajili ya kuzolea takataka, wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya magari hayo iliyofanyika kwenye ofisi za kampuni hiyo Barabara ya Nyerere Dar es Salaam.
Meya wa Ilala, Jerri Slaa, akizungumza wakati wa hafla hiyo.
http://sufianimafoto.blogspot.com/

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...