Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, March 27, 2011

MATUKIO MBALIMBALI YA TUZO ZA KILI

Mchezaji wa timu ya Simba Juma Kaseja Akimkabidhi tuzo ya nyimbo bora ya mwaka kwa msanii Mzee Yusufu kulia na Shedrak Msajigwa wa Yanga
Wasanii wa Muziki wa kizazi kipya wakiimba wakati wa onesho la tuzo za muziki nchini zilizoandaliwa na Kampuni ya bia nchini 'TBL' kupitia bia yake ya Kilimanjaro kutoka (kushoto) ni Ali Kiba, Banana Zoro na Nassib Abdul ‘Diamond’
Mashabiki Wakishangilia tuzo hizo
Mussa Hassani Mgosi wa Simba kushoto na Jerson Tegete wa Yanga kulia wakimkabidhi tuzo ya video bora ya mwaka msanii Khalfan Ilunga CPWA
Saidi Mabera akishangilia tuzo hiyo
Saidi Mabera akikunguta gita la Solo wakati wa tuzo hizo
Msanii Cpwaa akitoa shukrani zake za dhati kwa mashabiki wake walioweza kumpigia kura mpaka kuweza kupata tuzo ya Video Bora ya Muziki ya Mwaka.Cpwaa pia amechukua tuzo nyingine ya Ragga/Dancehall.
Tuzo ya Wimbo Bora wa Reggae ilienda kwa Hardmad.
Mbungu wa Viti Maalum wa CCM,Mh. Vicky Kamata akimkabidhi tuzo ya Wimbo Bora wa R&B msanii Ben Poul.
Msanii wa vichekesho toka kundi la Orijinal Comedy,ambaye pia ni Mwanamuziki akitoa shukrani zake kwa mashabiki wake waliomuwezesha kupata tuzo ya Wimbo Bora wa Asili wa Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...