Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, March 27, 2011

Ziara ya Makamu wa Rais Wilayani Magu


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Mohamed Gharib Bilal, akikata utepe kufunguwa Shule ya Sekondari Kitumba katika kijiji cka Kisesa Wilayani Magu wakati alipokuwa kwenye mfululizo wa ziara yake ya kukaguwa na kuzinduwa miradi ya maendeleo Mkoani Mwanza leo, Makamu wa Rais ameahidi kuchangia jumla ya shilingi milioni tatu kwa ajili ya kuanzisha utengenezaji wa miundombinu ya uvunaji wa maji ya mvua Shuleni hapo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Mohamed Gharib Bilal, akizungumza na Wananchi wa kijiji cha Kabila Wilayani Magu baada ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la upasuaji mdogo katika kituo cha Afya Kabila leo, Makamu wa Rais yupo Mkoani Mwanza kwa ajili ya kukaguwa na kuzinduwa miradi ya maendeleo ya Wananchi.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...