Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, October 31, 2012

Barnaba: Sijutii kwa niliekuwa nae



Na Elizabeth John
MKALI wa muziki wa kizazi kipya nchini, Barnaba Elias ‘Barnaba’ ameachia kibao chake kipya kinachokwenda kwa jina la ‘Sijutii kwa niliekuwa nae’.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Barnaba alisema wimbo huo kaupeleka sokoni wiki iliyopita na kwamba imeshaanza kufanya vizuri katika soko hilo, kitu ambacho kinampa moyo wa kufanya kazi hiyo.
“Kama kawaida yangu nyimbo zangu nyingi huwa haziwachukizi mashabiki wangu ni jambo ambalo namshukuru mungu kwani ni wasanii wachache ambao nyimbo zao zinafanya vizuri mtaani,” alisema.
Barnaba alisema anawaomba mashabiki wa muziki huo kuendelea kumpa sapoti katika kazi zake ikiwa ni pamoja na kukaa mkao wa kula kwaajili ya kuzipokea kazi nyingine.
Mbali na kibao hicho, Barnaba alishawahi tamba na vibao vyake kama, Magubegube, Wrong number, Tulizana, Milele daima na nyinginezo ambazo zinafanya vizuri katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya nchini.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...