Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, October 19, 2012

JWTZ YAINGIA KUTULIZA VURUGU ZA WAISLAMU KARIAKOO



 Mgambo na mashushushu  wakimdhibiti mmoja wa vijana waliokamatwa katika vurugu za Waislamu waliokuwa wakiandamana Kariakoo, Dar es Salaam leo, kulishinikiza Jeshi la  Polisi kumuachia huru Katibu wa Taasisi na Jumuia za Kiislamu, Issa Ponda ambaye ameshitakiwa yeye na wenzie kwa kuhamasisha vurugu.
Baadhi ya vijana wanaodaiwa kuwa wa kiislamu wakiahamasishana kuandamana leo katika BARABARA YA mSIBAZI, Kariakoo, Dar es Salaam, kwenda Makao Makuu ya Jeshi la Polisi kushinikiza Issa Ponda kuachiwa.
Askari Kanzu wakimshughulikia mmoja wa vijana wakati wa vurugu hizo
                                            Askari Kanzu akimdhibiti mtuhumiwa
                                Wanajeshi wakiwa kwenye Lori lao wakiasili kutuliza ghasia Kariakoo
                              Baadhi ya watuhumiwa wakiwa kwenye gari wakipelekwa kituo cha polisi
                           Mwendesha pikipiki akiwa chini ya ulinzi
                               Askari Kanzu akimdhibiti kijana aliyenaswa wakati wa vurugu hixo

                                                              Polisi wakiwa doria mitaa ya Kariakoo
                               Wanajeshi wakiungana na askari kanzu katika operesheni hiyo
                                                 Ni kasheshe kwenda mbele
                                       Mwanamama akiwa chini ya ulinzi
                                                          Wanahabari wakiwa kazini katika vurugu hizo

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...