Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, October 31, 2012

IZO ZILIPENDWA YA MATONYA VIDEONI




Na Elizabeth John
BAADA ya kufanya vizuri na wimbo wake wa ‘Taxi bubu’, Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini, Seif Shaban ‘Matonya’, ameachia video ya kibao chake cha ‘Izo Zilipendwa’ kinachofanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio.

Akizungumza jijini Dar es Salaama jana, Matonya alisema anamshukuru Mungu kibao chake kufanya vizuri kwani ni dalili nzuri ya kazi zake kukubalika, hivyo kuwaahidi wapenzi na mashabiki wake mambo mazuri zaidi.

“Kiukweli kazi hii imefanya vizuri, kitu ambacho kinanipa matumaini katika ‘game’ na natumaini video hii itakuwa bora zaidi,” alisema Matonya.

Matonya amewasihi mashabiki wake kukaa mkao wa kula kukisubiri kibao hicho na kwamba yuko katika hatua za mwisho za uandaaji wa kibao hicho.

Mbali ya kibao hicho, Matonya amewahi kutamba na vibao mbalimbali mahiri kama ‘Anita’,  ‘Vaileth’ na vinginevyo ambavyo vilimtambulisha kwa wapenzi na mashabiki wa muziki wa kizazi kipya.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...