Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, October 31, 2012

DROO YA PILI YA SHINDA NOAH YAFANYIKA, WASHINDI WAZIDI KUPATIKANA




Mshindi wa Kompyuta aina ya Dell, Rehema Kigadye wa Tegeta akiwa amepozi na zawadi yake.
DROO ya pili ya Bahati Nasibu ya Shinda Noah inayoendeshwa na Kampuni ya Global Publishers wachapishaji wa magazeti ya Ijumaa Wikienda, Uwazi, Risasi, Amani, Ijumaa na Championi leo imewapata washindi wengine katika Viwanja vya Karume, jijini Dar.
Meneja mkuu wa Global, Abdallah Mrisho (kulia) akimkabidhi zawadi mmoja wa washindi wa papo kwa papo.
Washindi waliopatikana katika droo hiyo na kujinyakulia zawadi tofauti ni, Rukia Vitali wa Boko, Dar (TV Flat Screen), Leah Andrew wa Mwananyamala (Simu aina ya Samsung Galaxy), Rehema Kigadye wa Tegeta (Jezi) huku wengine wakijinyakulia zawadi za papo kwa papo (kama wanavyoonekana pichani).
Mfanyakazi wa Global, Jimmy akimwelekeza mshiriki namna ya kujiunga kwenye shindano.
Droo ikichezeshwa.
Afisa Masoko wa Global, Benjamini Mwanambuu (kulia) akimkabidhi zawadi ya T- shirt mmoja wa washiriki waliojitokeza.

(PICHA/HABARI: ERICK EVARIST/GPL)

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...