Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, August 13, 2013

JIMMY MASTER NA HEKAEKA ZA UJIO WA DOUBLE J


YULE muongozaji na mwigizaji Jimmy Mponda 'Jimmy Master' aliyetikisa
 na mfululizo wa filamu za misuko iliyotoka sehemu ya kwanza hadi ya
tatu na baadaye kujiongezea jina lingine akiitwa J Plus.
Jimmy Master
Kwa sasa nyota huyo amefunguka  kuwa yukombioni kutoa muvi ya mwisho
inayoitwa Doble J Final  huku ujio huo ukiwa ni wa mwisho kutoka baada
ya kutangulia  na Doble J sehemu ya kwanza na yapili zilizotoka mwaka jana.

"Mwaka jana nilifanikiwa kukonga nyoyo za mashabiki wa filamu hususani
 wanaopagawa na filamu za mapigano na kujawa mambo ya  kipelelezi,"alisema J Plus.

Alisema Doble J Final pia ni ujio wake wa filamu nyingine ya mapigano na
 kuna heka heka za kipelelezi ndani. J Plus aliyezoeleka sasa katika kuonesha
ubabe wa kufa mtu , kwa sasa ujio wake huo unao tazamiwa kuingia sokoni mapema tu ,
 mwezi ujao .
Pia Jimmy Master amemshirikisha mbabe mwingine katika filamu za mapigano Ibrahim Mbwana  'Bad Boy'
na pia wamo nyota wengine katika dulu la filamu kama Charles Magari , Hashim Kambi na
Veronica Viankero.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...