Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, October 5, 2012

WAZIRI WA FEDHA AZINDUAHUDUMA YA FARAJA BIMA KUPITIA M-PESA





 Waziri wa fedha Dk. William Mgimwa akiongea wakati wa uzinduzi wa kutumia huduma ya Faraja Bima kupitia M-pesa kwa kushirikiana na Heritage Insurance, uzinduzi huo ulifanyika jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi mtendaji wa Vodacom Tanzania Bw. Rene Meza akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa huduma ya Faraja Bima itakayopatika kupitia M-pesa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Heritage Insurance Bw.Paul Lewis akisema machache wakati wa uzinduzi huo.
Meneja Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Bi.Rukia Mtingwa kushoto akimsikiliza jambo Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo Bw.Matina Nkurlu, watatu toka kushoto wakati wa uzinduzi wa kutumia huduma ya Faraja Bima kupitia M-pesa,wapili kutoka kushoto ni Meneja Mahusiano ya nje wa Vodacom Tanzania Bw.Salum Mwalim na kulia ni Angela Sompet.
Ofisa Mkuu wa M-Biashara wa Vodacom Jacques Voogtz (Katikati) akimuonyesha Waziri wa fedha Dk. William Mgimwa namna ya kujiunga na kutumia huduma ya Faraja Bima kupitia M-pesa baada ya kuizindua jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza. Kupitia Faraja bima mteja anweza kulipia bima yake kwa M-pesa.
---
 Huduma ya Vodacom ya M-Pesa imezidi kupiga hatua baada ya kuwawezesha Watanzania kufanya malipo yao ya bima kupitia huduma hiyo.
 
Hii inafuatia ushirikiano kati ya Vodacom Tanzania na Heritage Tanzania kuzindua Bima ya Faraja, ambayo ni Bima ya mazishi ambayo inamuwezesha mlengwa kulipwa fedha taslim za mazishi kwa muhusika mwenye bima. Bidhaa mbalimbali ziko katika mpango huo ili kukidhi mahitaji ya wateja na bajeti ya malipo ya kila mwezi kuanzia shilingi 20000/= fadi 9800/= kwa Mwezi.
Mteja ana chaguo la kuongeza malipo kwa kuongeza huduma ya vifo vinavyotokana na ajali kulingana na faida na sera zao. Ongezeko hili la ziada litaongeza kiasi cha faida mara tatu kwa ongezeko dogo la malipo. 
Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania, Rene Meza, amesema wateja wa Vodacom wanaotumia M-Pesa, wataweza kujipatia bima ya bure kwa mwezi. 
“Wateja wetu wote ambao watafanikiwa kutuma pesa walau mara 10 kwa Mwezi watapata  bima ya bure ya kiasi cha Shilingi laki mbili kwa mwezi unaofuata,” amesema Meza.
Suala la kipekee katika huduma hii ni kwamba hakuna haja ya kujaza fomu ili kujiunga na bima hii. Mteja atajiunga kwa njia rahisi kwa kupiga *150*00# na kuchagua kipengele cha bima. Vodacom inahakikisha kuwa wateja wote wa M-pesa wanaweza kupata huduma hii ili kuwa na amani ndani ya familia zao.
 “Ni muhimu kuthibitisha kuwa taarifa zako ni sahihi, na kuthibitisha kuwa unaelewa vigezo na masharti. Taarifa zako zitatumwa moja kwa moja kwenda Heritage Tanzania,” alisema Meza na kuongeza kuwa, “Unaweza kuchagua aina ya bima ambayo inakidhi mahitaji na bajeti yako,”
Bima hii ya Faraja pia itawawezesha kila mmoja kubadili au kuongeza kiwango chake kwa ile yenye faida zaidi kulingana na mahitaji yao na mabadiliko ya bajeti katika maisha yao.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...