Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, January 17, 2013

Mshindi ‘Valentine Day’ kulamba Vitz



Meneja Mauzo na Masoko wa Push Media Mobile, Rodney Rugambo akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa shindano la kampeni maalum ya kuadhimisha sikukuu ya wapendanao ‘ Valentine Day’ iliyoandaliwa kwa kushirikiana na Kampuni ya African Media group (AMG) kupitia kituo cha televisheni cha Channel Ten na Redio Magic FM. Kushoto ni AFISA Masoko na Mauzo wa AMG,  Prosper Vedasto 


Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Push Media Mobile inatarajiwa kutoa zawadi ya gari aina ya Vitz lenye thamani ya sh milioni 8 kwa mshindi wa kampeni maalum ya kuadhimisha sikukuu ya wapendanao ‘Valentine Day’ inayoadhimishwa Februari 14 kila mwaka.

Hayo yalisemwa jijini Dar es Salaam Meneja Mauzo na Masoko wa Push Media Mobile, Rodney Rugambo, katika uzinduzi wa kampeni hiyo pamoja na Kampuni ya African Media Group (AMG), kupitia kituo cha televisheni cha Channel Ten na Redio Magic FM.

Rugambo alisema kuwa, wameamua kutoa zawadi hiyo kubwa ili kuwafanya wapendanao wengi kushiriki na kupata nafasi ya kushinda.

Alisema kuwa, ili kuingia katika droo ya shindano hilo, unatakiwa kutuma neno ‘Penzi’ kwenda namba 15678 na kujibu maswali mbalimbali yahusiyo masuala ya mapenzi na siku ya Valentine.

“Hii ni promosheni ya kwanza kubwa hapa nchini na mshindi kujishindia gari, lengo kubwa ni kutoa ufahamu kuhusiana na sikukuu ya wapendanao na vile vile kuwazawadia wadau wetu kwa kushiriki katika shughuli zao za ujenzi wa taifa,” alisema Rugambo.

Alisema kuwa, mbali ya zawadi hizo, washiriki wa promosheni hiyo pia watapata nafasi ya kujishindia kompyuta (Laptop), aina ya HP yenye thamani ya sh milioni 1.5, simu aina ya Blackberry Curve yenye thamani ya sh 500,000 na ‘Home Theatre’ ya thamani ya sh 400,000.

Kwa mujibu wa Rugambo, lengo lao kubwa ni kuifanya sikukuu ya wapendanao kuwa kubwa kama nyingine, kwani mapenzi ni kitu muhimu katika maisha ya kila siku.

Alisema kuwa, mipango yao ni kuwekeza katika sikukuu hiyo, ambayo jamii imeanza kuitilia mkazo japo si siku ya mapumziko kama sikukuu nyingine, ambako mwaka huu, wameweka bajeti ya sh milioni 30 ili kufanikisha zaoezi hilo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...