Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, January 17, 2013

PNC KUFANYA MAGEUZI KATIKA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA



Na Elizabeth John
BAADA ya kimya cha muda mrefu, msanii wa muziki kizazi kipya, Pancras Ndaki Charles ‘PNC’, ameibuka na kusema amerudi kufanya mageuzi makubwa katika muziki huo na kumtaka msanii mwenzake Naseeb Abdul ‘Diamond Platinum’ ajiandae kuvaa vumbi.

Akizungumza na Habari Mseto Blog, PNC, amesema kuwa ukimya wake haukuwa bure bali alikuwa anajipanga vema na ujio wake mpya umekuja huku Diamond akioneka kuliteka anga la muziki huo na kumtambia kuwa muda si mrefu atamfunika.

“Nilikaa kimya muda mrefu baada ya kutamba na ngoma yangu ya ‘Mbona’ niliyomshirikisha Mr Blue, na kipindi chote nilikuwa najaribu kuangalia jinsi nitakavyoliteka anga la muziki huu, na ujio wangu mpya umekuja wakati Diamond akiwa safi, hivyo asubiri kuvaa vumbi kwani nitampoteza vibaya,” alisema PNC.

PNC anayesimamiwa na meneja wake makini, Ostaz Juma, chini ya lebo ya Mtanashati Entertainment, alisema hivi karibuni anatarajia kuachia ngoma yake mpya ambayo hajataka kuitaja jina kutokana na maharamia waliopo katika tasnia hiyo.

Mmsanii huyo ambaye ndiye kiongonzi wa kundi la Mtanashati Entertainment, anawaomba wadau na mashabiki wa muziki huo kukaa mkao wa kula kwaajili ya kuzipokea kazi zao zinazokuja.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...