Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, January 17, 2013

Nay Wa Mitego: Nasema Nao ni hisia zangu binafsi



Na Elizabeth John
MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ amesema wimbo wake wa ‘Nasema Nao’, ambao unafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio na runinga, ni hisia zake binafsi na wala hana bifu na mtu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Nay, alisema kuwa alifanikiwa kurekodi wimbo huo baada ya kufika studio na kukuta mapigo bila wimbo, na ndipo alipoamua kufanyia mazoezi kabla ya kuirekodi na kuisambaza.

Nay, alisema hakukusudia kumsema mtu, licha ya baadhi ya maneno ya wimbo huo kuwa na majina ya wasanii na viongozi, lakini lengo lake ni kufikisha ujumbe kwa jamii na si vinginevyo.

“Mimi ndiye msanii wa kwanza wa muziki wa kizazi kipya kutaja watu kwenye nyimbo nikiwa na lengo la kufikisha ujumbe ninaoukusudia kwa jamii, na humu simaanishi chochote kibaya,” alisema Nay Wa Mitego.

Mkali huyo wa Bongo Fleva, alisema katika hilo, hana ‘bifu’ na mtu yeyote na hatarajii kusikia akiingia katika malumbano na wasanii waliotajwa katika wimbo huo ambao unafanya vizuri katika redio mbalimbali nchini.

Baadhi ya wasanii waliotajwa katika wimbo huo ni pamoja na Selemani Msindi ‘Afande Sele’,  Hamad Ally ‘Madee’, Chid Benzi na viongozi wengine wa kisiasa.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...