Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, January 17, 2013

MZEE MALECELA, WAZIRI MKUU MSTAAFU SUMAYE NA JAJI MKUU MSTAAFU SAMATTA WATOA MAONI KATIBA MPYA LEO



Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye akiongea na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliokutana nao leo kutoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Tume Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani na Mjumbe wa Tume Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Salim Ahmed Salim (katikati).
Jaji Mkuu Mstaafu Barnabas Samatta akiongea na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliokutana nao leo kutoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya. Kulia ni Mwenyekiti wa Tume Jaji Joseph Warioba.
Waziri Mkuu Mstaafu Mzee John Malecela akipata maelezo kuhusu Kitengo cha Utafiti cha Tume ya Mabadiliko ya Katiba kutoka kwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume Bw. Mohammed Hamad leo mara baada ya kutoa maoni yake kuhusu katiba Mpya. Kushoto ni Mwenyekiti wa Tume Jaji Joseph Warioba.
Waziri Mkuu Mstaafu Mzee John Malecela akiongea na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliokutana nao leo kutoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya. Kulia ni Makamu Mwenyekiti Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani na Mjumbe wa Tume Prof. Mwesiga Baregu.
Waziri Mkuu Mstaafu Mzee John Malecela akitoka nje ya ukumbi wa mikutano wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba leo mara baada ya kutoa maoni yake kuhusu katiba Mpya. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani na kulia ni Mjumbe wa Tume Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Salim Ahmed Salim.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...