Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, September 27, 2011

TUSKER MALT LAGER YADHAMINI TAFRIJA YA HISANI YA SHEAR KIASI CHA SH. MIL25


TUSKER MALT LAGER YADHAMINI TAFRIJA YA HISANI YA SHEAR
(Shear Charity Ball 2011)YENYE LENGO LA KUSAIDIA MRADI WA FISTULA KATIKA HOSPITALI YA CCBRT NA PIA KUWEZESHA KUKARABATI MFUMO WA MAJI KATIKA HOSPITALI YA AMANA
Kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya ShearIllusions Shekha Nasser ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Tafrija ya Shear Charity Ball 2011, katikati ni Ofisa wa Mahusiano ya Jamii Kampuni ya Bia Serengeti (SBL), Nandi Mwiyombela na Ofisa wa Idara ya Mambo ya Ndani SBL Imani Lwinga wakizungumza na waandishi leo asubuhi katika ofisi zao zilizopo Oysterbay Dar es Salaam.
KAMPUNI ya Bia ya Serengeti imetangaza kutoa udhamini mnono kwa katika kuchangia na kufanikisha tafrija ya ‘Shear Charity Ball 2011’ itakayofanyika Jumamosi Oktoba mosi katika hoteli ya Movenpick, Dar es Salaam.
Akitangaza udhamini huo Meneja wa Mahusiano ya Jamii Kampuni ya Bia Serengeti Nandi Mwiyombela alisema.
“Kampuni ya Bia Serengeti ambao ndiyo wadhamini wakuu tuna kila sababu ya jivunia kutangaza kuwa tumechangia kiasi cha sh. mil 25 katika kufanikisha tafrija hii ambayo itaenda sambamba na chakula cha usiku pamoja muziki” alisema .
Alisema tafrija hii itaanza saa moja kamili jioni
Huku wageni walikwa wakiwa wametakiwa kuvaa katika mavazi yenye rangi nyeupe na nyeusi.
“Katika tafrija ya mwaka huu ambayo inafanyika kwa mara ya pili sasa imelenga kuchangisha kiasi cha sh.mil 50 kwa ajili ya taasisi mbili ambazo ni CCBRT na Hospitali ya Amana”alisema Mwiyombela.

Wakati huohuo Mwiyombela aliongeza kwa kusema kuwa leo wasanii wa kundi la Mutati kutoka nchini Kenya watawasili nchini ambapo watatoa burudani katika tafrija hiyo.

“Kesho usiku kutakuwa na muziki katika ukumbi wa Nyumbani Lounge na kiingilio kitakuwa sh.10,000 napenda kuwaeleza kwamba fedha hizo zitapelekwa katika kuchangia matibabu ya upasuaji kwa wagonjwa wa Fistula katika hospitali ya CCBRT na kuweka mfumo wa maji safi na taka Amana
” alisema .

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...