Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, September 27, 2011

YOHANA ROBART KUTETEA UBINGWA WAKE



BINGWA wa mkanda wa TPBO Yohana Robert amechezea kichapo kutoka kwa Jonas Godfrey katika pambano lake la maandalizi la kutetea ubingwa huo lililofanyika juzi katika ukumbi wa DDC Magomeni Dar es Salaam.

Kutokana na kichapo hicho Robert atakuwa amejipunguzia heshima ya kutetea ubingwa huo ambao anatarajia kuutetea Septemba 30 mwaka huu jijini Tanga kwa kutwangana na bondia Alan Kamote.

Awali Robert alitakiwa kutwangana na Mohamed Shaaban ambaye hakutokea siku ya kupima uzito hivyo kumfanya Robert kubadilishiwa mpinzani katika dakika za mwisho.

Akizungumzia kichapo hicho Kocha wa Robert, Rajab Mhamila alisema kitendo cha bondia wake kubadilishiwa mpinzani ndicho kilichopelekea kichapo kwa bondia wake.

"Mimi sijafurahishwa kabisa bondia wangu kupigwa kwa sababu imempunguzia heshima ya ubingwa wake pia kitendo cha Shaaban kuingia mitini nacho pia kimenikera kwa kuwa tulitegemea ndiye bondia atakayecheza nae,"alisema Mhamila.

Alisema hata hivyo mapungufu yaliyojitokeza kwa bondia wake atayafanyia kazi ili aweze kufanikiwa kuutetea mkanda huo jijini Tanga.

Bondia Robert alipigwa na Godfrey kwa pointi 40-39 ambapo pambano lao lilikuwa la raundi sita. aliongeza kuwa atatumia nafasi ya kumpereka bondia wake tanga na kuamasisha mchezo wa ngumi kupitia DVD zake za Super D Boxing Coach zinazoelekeza mafunzo ya mchezo huo

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...