Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, February 18, 2012

AIRTEL YATOA MAFUNZO KWA MAWAKALA JUU YA HUDUMA YA AIRTEL MONEY






Afisa mauzo wa Airtel Tanzania kitengo cha Airtel Money Bahati Straton akitoa mafunzo kuhusu huduma ya Airtel money kwa mawakala mbalimbali kutoka Mkoa wa Dar es Saalam lengo likiwa ni kuwaelimisha wadau hawa kuhusu huduma ya pesa mkononi na kuboresha uelewa wa huduma hiyo kwa watumiaji na wafanyabiashara, semina hiyo ilifanyika katika makao makuu ya Airtel Morroco.


Bwana Abdallah Litumbui wakala wa Airtel money Msimbazi Kariakoo akiuliza swali juu ya huduma ya Airtel Money wakati wa seminar ya Airtel money iliyoandaliwa ikiwa na lengo la kuwaelimisha mawakala zaidi kuhusu huduma ya Airtel Money , semina hii iliyofanyika katika makao makuu ya Airtel Moroco na kuhudhuriwa na mawakala wengi kutoka Dar es Saalam.


Bwana Salim Mwinyimanzi wakala wa Airtel money Kibada Kibagomboni akichangia hoja kuhusu huduma ya Airtel Money wakati wa seminar ya Airtel money iliyoandaliwa kwa lengo la kuwaelimisha mawakala zaidi kuhusu huduma ya Airtel Money , semina hii iliyofanyika katika makao makuu ya Airtel Moroco na kuhudhuriwa na mawakala wengi kutoka Dar es Saalam.

1 comment:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...