Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, October 17, 2011

RAIS DK. JAKAYA KIKWETE AWASILI MPANDA NA KUZINDUA MKUTANO WA UWEKEZAJI UKANDA WA ZIWA TANGANYIKA


Rais Dk. Jakaya Kikwete akisaliaiana na Waziri mkuu Mh. Mizengo Pinda, mara baada ya kuwasilia katika uwanja wa ndege wa Mpanda leo asubuhi, tayari kwa kufungua mkutano wa uwekezaji katika ukanda wa ziwa Tanzaganyika mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma unaohudhuriwa na Mabalozi, maofisa wa serikali na wafanyabiashara pamoja na wawekezaji wa ndani na wa nje ya nchi, mkutano huo hivi sasa unaendelea kwenye ukumbi wa idara ya maji mjini Mpanda. Mpaka sasa Rais tayari ameshaingia ukumbini na anaendelea na hotuba yake ya ufunguzi matukio zaidi ya ufunguzi wa mkutano huo yatawajia baada ya muda, katika picha kulia anayeshuhudia ni Mkuu wa mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya.
Rais Jakaya Kikwete akilakiwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Mkuu wa mkoa wa Rukwa Injini Stella Manyanya, mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mpanda.
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Waziri wa Uchukuzi Omar Nundu wakati alipowasili katika uwanja wa ndege wa Mpanda.
Wageni mbalimbali wakiwemo mabalozi pamoja na wawekezaji wakiwasili katika uwanja wa ndege wa Mpanda.
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Rajabu Rutengwe katikati akiwaelekeza wageni mbalimbali wakati waliposili kwenye uwanja wa ndege mjini mpanda leo asubuhi kwa ajili ya mkutano huo.
picha na habari kwa hisani ya http://fullshangwe.blogspot.com/

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...