Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, May 21, 2012

Print conversation Print Open conversation in new window New window WAKULIMA WA KILIMO CHA KISASA KUTOKA NCHINI AFRIKA KUSINI WATEMBELEA TANZANIA

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Africa Century 4 Development (CC) Fred Simon akizungumza na waandishi wa habari pamoja na kuwakaribisha wakulima wa kilimo cha kisasa kutoka makampuni 13 ya nchini Afrika Kusini ambao wamekuja Tanzania kwa ajili ya matembezi ya kujifunza mbinu mbali mbali za kilimo na kuangalia fulsa za kuikwamu Tanzania katika mpango wa kilimo kwanza.
Bw. Simon alisema kuwa kilimo ni biashara inayolipa kwa kiasi kikubwa, hivyo ni vyema kila mmoja wao kufanya kazi kwa bidii.
Mkutano wa waandishi wa habari pamoja wakulima wa kilimo cha kisasa kutoka Afrika Kusini.
Wageni wakifuatilia mkutano huo.
Katibu Mtendaji wa Tanzania Youth Agriculture Foundation (TYAF) Bw. Gasper Mahekula akitoa maelezo machache ya taasisi yao mbele ya wakulima kutoka nchini Afrika Kusini pamoja na waandishi wa habari ambapo aliwakaribisha wageni hao kuwekeza katika kilimo.
Wa kwanza kulia ni Mtaalam wa Mambo ya Utawala wa Kilimo wa Kampuni ya IIQ ya Afrika Kusini Bw. Ockie Olivier ambaye ameongozana na wenzake wakifuatilia mkutano huo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Konsortium, Afrika Kusini Bw. Braam Coetnee (kushoto) wakiwa na mmoja ya wenyeji wao (katikati) pamoja na Kiongozi anayehusika na mambo ya nje ya Kampuni ya Konsortium, Afrika Kusini Bw. John Luscombe jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Africa Century 4 Development (CC) Fred Simon akifanya mazungumzo na waandishi wa habari mara baada ya mkutano jijini Dar es Salaam.
Kiongozi anayehusika na mambo ya nje ya Kampuni ya Konsortium, Afrika Kusini Bw. John Luscombe akifanya mahojiano na waandishi wa habari mara baada ya mkutano jijini Dar es Salaam. Picha/www.kajunason.blogspot.com


----
Cathbert Angelo Kajuna,
Founder and Mananging Director
Kajunason Blog,
P.O Box 6482,
Dar es Salaam.
Tel: +255 713 797 465
"Everything is Possible Through Peace & Stability''

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...