Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, May 30, 2012

WAZIRI AMOS MAKALA AIKABIDHI BENDERA TIMU YA (TAIFA TAIFA STARS)


Naibu waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mh, Amos Makala akizungumza na waandishi wa habari leo hii jijini Dar es Salaam wakati akikabidhi bendera kwa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars inayokwenda Nchini Ivory coast kucheza na timu ya taifa ya nchi hiyo  jumamosi ya wiki hii ambapo aliwataka wachezaji wa timu hiyo kuipa raha Tanzania kwa kishindo kizito na kuwatangazia kuwa wasiogope wachezaji wa Ivory coast makabidhiano hayo yamefanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Tansoma jijini Dar es Salaam.
(PICHA NA PHILEMONI SOLOMON WA FULLSHANGWE)
Rais wa shirikisho la Mpira Tanzania TFF Bw, Leodger Tenga akiwatakia wachezaji hhao kila la heri katika safari yao na kuwatakia ushindi mwema.
Kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars Kim Paulsen akiwahakikishia watanzania kuwa watakwenda kule Ivory Coast  kushinda kwani amewafundisha wachezaji wake namna ya kujiamini wenyewe na pia kuwa na nidhamu mchezoni ili waweze kupata ushindi.
Wachezaji wa timu ya Taifa waliohudhuria katika Tafrija hiyo ya kukabidhiwa Bendera.
Naibu waziri wa Utamaduni na Michezo Mh, Amos Makala (kushoto) akimkabidhi bendera ya taifa kapteni wa timu hiyo Mlinda mlango Juma Kaseja.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...