Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, February 15, 2013

HUSEIN MACHOZI AMFANANISHA DIAMOND NA KUKU JIKE

HUSEIN MACHOZI
‘Addicted hit maker’ Hussein Machozi amefunguka kuhusu uhusiano wake na Diamond platnumz na kuonesha kuwa hawana urafiki hata kidogo, japo hakusema moja kwa moja kama wana uadui na kwamba yeye na Diamond ni kama ‘Jogoo na kuku Jike’ na yeye Hussein ndiye jogoo!


Hussein Rashid a.k.a Hussein Machozi amefunguka kwenye XXL ya Clouds fm katika segment ya U Heard, alipotakiwa kutoa ufafanuzi kuhusu tuhuma zilizowafikia ‘Timu Makorokocho’ kuwa Hussein Machozi alipigana na Diamond Platinumz huko Mombasa.


Japo Hussein alikiri kuwa anauwezo wa kupigana kama bondia, lakini alikanusha kabisa kuwa hajawahi kupigana na Diamond na wala hajawahi kuzinguana nae, kwa sababu hawajawahi kabisa kuwa karibu, na sababu ni kwamba wanatokea katika sayari tofauti kabisa, yeye anatokea sayari nyingine na hajui Diamond anatokea sayari gani.


Japo aliongea kwa ufupi sana lakini hii ilitoa picha ya moja kwa moja kuwa inawezekana Hussein ana kitu moyoni ama hasira flani kuhusu Diamond Platinumz. Je wewe unamtazamo gani kuhusu hili?


DIAMOND

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...