Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, February 25, 2013

SERIKALI INATAMBUA KATIBA YA 2006 YA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI (TFF)



WAZIRI WA HABARI, MICHEZO, UTAMADUNI NA VIJANA, FENELLA MUKANGARA.

Waziri wa habari, michezo, utamaduni na vijana, Fenella Mukangara amefuta matumizi ya katiba mpya ya TFF ya mwaka 2012 kwa vile imekiuka kanuni na sheria za BMT hivyo TFF wanatakiwa kutukia katiba ya mwaka 2006 ambayo imetumika katika mikoa kufanyia uchaguzi.
Mukangara amesema TFF inatakiwa kufuata kanuni nasheria za BMT ambazo ambazo ndizo zenye maelekezo ya kufanya marekebisho ya katiba .

Hakuna chama chochote hapa nchini kilicho juu ya BMT yaani baraza la michezo nchini ,hivyo TFF wanatakiwa kufanya mkutano mkuu kwa kutumia katiba ya mwaka 2006 na FIFA wanatakiwa kuelezwa mambo yalivyo pindi watakapokuwa hapa.

Pia waziri amesema anamuondoa kazi msajili aliyepitisha katiba ya TFF kwani hajafuata kanunu na sheria na kumuweka mwingi pamoja na kuhamisha ofisi ya msajili

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...