Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, February 20, 2013

WANAFUNZI WAKUTWA MAFICHONI KAMA WAHAMIAJI HARAMU KUKWEPA UKAGUZI WA KUSHITUKIZA WA MKUU WA WILAYA


Mkuu wa wilaya ya Ilemela Bi. Amina Masenza akishuhudia mlundikano wa magodoro na hali ya  sehemu wanayolala wavulana wa shule ya Mount Zion kwenye moja ya vyumba vya darasa vilivyotengwa kwa ajili ya kujisitiri.
ZIARA ya kushitukiza iliyofanywa na Mkuu wa wilaya ya Ilemela Bi. Amina Masenza akiambatana na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama kufanya ukaguzi katika shule ya sekondari ya Mount Zion iliyoko ilemela jijini Mwanza imebaini wanafunzi kuishi katika mazingira hatarishi huku uongozi wa shule hiyo ukiwaficha vichakani zaidi ya wanafunzi 50 wa bweni kukwepa ukaguzi. 

Hatua hiyo inafuatia kuwepo taarifa zilizotolewa kwa mkuu huyo na baadhi ya wasamaria wema hali iliyomlazimu mkuu wa wilaya na ujumbe wake kufika shuleni hapo ili kujionea endapo uongozi wa shule hiyo umeboresha kasoro na mapungufu yaliyoonekana baada ya ukaguzi wa awali kufanyika kwa kipindi cha mwezi mmoja uliopita baada ya kutakiwa kuyafanyia kazi mapungufu hayo na Idara ya Afya na Elimu ukaguzi.
Mkuu wa wilaya ya Ilemela Bi. Amina Masenza  alishuhudia jinsi hali mbaya kwa vyoo vilivyounganishwa ndani ya bweni njia zikiwa zimebananishwa na masanduku ya bati ya kuhifadhia nguo za wanafunzi bila kuwa na usalama wa kiafya.
Wanafunzi  50 waliobainika kufichwa waumbuliwa.
Hata hivyo jeshi la polisi baada ya kupata taarifa hizo nalo lilifuatilia na kufanya msako kwenye vichaka vinavyozunguka shule hiyo na kufanikiwa  kuwakuta wanafunzi hao wakiwa wamejificha chini ya ulinzi wa mmoja kati ya waalimu wa shule hiyo kisha kuwaamuru kwenda shuleni ambapo mkuu wa wilaya na ujumbe wake walikuwa wakizungumza na uongozi wa shule na wanafunzi wengine hali iliyo washangaza.
Msafara wa wanafunzi wa kidato cha kwanza waliojificha na mwalimu wao kukwepa kukutwa wakiwa wamekalia ndoo kwenye msongamano madarasani ukirejeshwa shuleni chini ya uangalizi wa maafisa wa jeshi la polisi nyuma na mbele ya msafara.
Akizungumza huku machozi yakimbubujika kwa uchungu wa hali aliyoishuhudia shuleni hapo Mkuu wa wilaya ya Ilemela Bi. Amina Masenza ameeleza kusikitishwa kwa kitendo hicho na kukilaani vikali akiagiza hatua madhubuti za kisheria kuchukuliwa dhidi ya Mkurugenzi wa shule hiyo….
Msikilize kwa kubofya play..



Hii ndiyo hali halisi ya ukaaji ndani ya darasa hili jeh kwa mpango huu  kuna usalama wa kufanya vyema  kazi za darasani na hatimaye kufaulu kwenye mitiani kihalali? Kwa Picha Zaidi BOFYA HAPA

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...